KISA SARE NA AZAM JANA...SIMBA WAVUNJA UKIMYA TAMKO LAO HILI HAPA


Hakimiliki ya picha: Soka La Bongo 


BAADA ya Februari 24 2025 ubao wa Uwanja wa Mkapa kusoma Simba 2-2 Azam FC mabosi hao wakigawana pointi mojamoja na matajiri wa Dar, Azam FC, Simba wametoa tamko lao kuhusu aina ya matokeo hayo.
 
Kupitia kwenye ukurasa wa Instagram wa Ahmed Ally ambaye ni Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba ameandika namna hii: Sare dhidi ya Azam FC isitufanye tujitoe kwenye mbio za ubingwa sisi wenyewe.
 
Pamoja na kwamba matokeo yametuumiza lakini yasiwe ni matokeo ya kutukatisha tamaa kwenye kupigania malengo yetu ya msimu.
 
“Tumepata sare dhidi ya timu bora na mshindani wa kweli hivyo hatuna sababu ya kukaa kinyonge. Tusiiinamishe vichwa chini mapambano yaendelee tena kwa kujiamini kwani nafasi ya mafanikio ni kubwa sana kwetu
 
“Ubaya Ubwela hauna side Mirror hivyo hatuna budi kuangalia nyuma tunapaswa kusonga mbele kwa mwendo wa ngiri. Tuna michezo 10 imesalia hii ni kufa na kupona, tunapaswa kushinda michezo yote na hilo tunaliweza,
 
“Mafanikio yetu msimu huu yapo kwenye mechi hizi 10. Nichukue nafasi hii kuwaomba Wana Simba, tuachane na kilichopotea tujikite kwenye kutafuta kilicho mbele yetu.”


Jisajili na Betway, burudika na kila tukio na amsha amsha ukibashiri kwenye ligi za mpira wa miguu kama; Ligi Kuu ya Uingereza, La Liga, Ligi ya Mabingwa Ulaya na mengi zaidi.

Bashiri popote

Kwa habari zote za michezo, taarifa za kubashiri na promosheni tufuatilie Betway kwenye kurasa zetu za FacebookTwitterInstagram na Youtube. Pakua App ya Betway.
 

Published: 02/25/2025