Hakimiliki ya picha: Soka La Bongo
BEKI wa kazi ndani ya kikosi cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Miloud Hamdi, Ibrahim Bacca deni lake la mabao kwa sasa ni 11 ili kufanikisha malengo aliyokuwa nayo msimu wa 2024/25.
Beki huyo mwanzo wa msimu baada ya kufungua akaunti yake ya mabao kwenye mchezo dhidi ya Ken Gold uliochezwa Uwanja wa Sokoine alibainisha kuwa anamalengo ya kuwa mfungaji bora.
Kwenye mchezo huo baada ya dakika 90 ubao ulisoma Ken Gold 0-1 Yanga bao la Bacca likiwa ni la ushindi kwa
Yanga inayoongoza ligi ikiwa na pointi
58 kibindoni.
Beki huyo alisema: “Nina malengo yakuwa mfungaji bora ambapo kwa ligi yetu namna ilivyo ukifikisha mabao kuanzia 15 una nafasi ya kutwaa kiatu cha ufungaji hivyo nina amini itakuwa hivyo kwangu pia.
“Inawezekana licha ya kwamba mimi ni beki bado ninauwezo wakufunga ndio maana unaona inakuwa hivyo, ninamshukuru Mungu kwa yote yanayotokea na ushirikiano ambao ninapata kutoka kwa wachezaji na benchi la ufundi.”
Kwa sasa kwenye ligi amefunga mabao manne akiwa ni beki namba moja mwenye mabao mengi, ni Tanzania Prisons timu ambayo aliifunga mabao mengi ambayo ni mawili Uwanja wa KMC, Complex.
Jisajili na Betway, burudika na kila tukio na amsha amsha ukibashiri kwenye ligi za mpira wa miguu kama;
Ligi Kuu ya Uingereza, La Liga, Ligi ya Mabingwa Ulaya na mengi zaidi.
Kwa habari zote za michezo, taarifa za kubashiri na promosheni tufuatilie
Betway kwenye kurasa zetu za
Facebook,
Twitter,
Instagram na
Youtube. Pakua App ya Betway.